Sonko Awaombea Wakenya Wanaomkejeli Wakisema Amekuwa Bloga

- Mike Sonko mnamo Disemba 3, 2020, alibanduliwa afisini na wawakilishi 88 wa wadi ya Nairobi kufuatia tuhuma za ukiukaji Katiba, matumizi mabaya ya mamlaka na utovu wa nidhamu - Mnamo Disemba 17, 2020, Seneti iliunga mkono uamuzi wa bunge la kaunti kumfukuza mwanasiasa huyo kazini

- Mike Sonko mnamo Disemba 3, 2020, alibanduliwa afisini na wawakilishi 88 wa wadi ya Nairobi kufuatia tuhuma za ukiukaji Katiba, matumizi mabaya ya mamlaka na utovu wa nidhamu

- Mnamo Disemba 17, 2020, Seneti iliunga mkono uamuzi wa bunge la kaunti kumfukuza mwanasiasa huyo kazini

- Baada ya kutimuliwa, mwanasiasa huyo alisema ana furaha ya kurudia maisha yake ya zamani kabla ya kujiingiza katika siasa

- Tangu wakati huo, amekuwa akichapisha kutia moyo kwenye kurasa zake za mitandao ya kijamii

Aliyejuwa Gavana wa Nairobi Mike Sonko amemwomba Mungu awasamehe Wakenya ambao wamemkejeli mtandaoni kwa machapisho yake ya kuliwaza na kutia moyo

Habari Nyingine: Magazeti Jumanne, Mei 4: Ziara ya Kwanza ya Samia Nchini Kenya Tangu kuwa Rais

Katika ujumbe aliochapisha mitandaoni Jumanne, Mei 4, mwanasiasa huyo mwenye utata alipuzilia mbali kwamba sasa amebadilishwa kuwa bloga baada ya kuondolewa mamlakani katika kiti cha ugavana wa Nairobi.

"Kwetu, shida huzingatiwa kama kitu cha maana kwa sababu hutufanya tuwe na nguvu na hekima. Wakati mwingine tunaposali wale ambao hawajui chochote kuhusu nguvu ya maombi haswa wakati wa shida wanasema tumeshushwa cheo na kuwa wanablogu kutokana na shida ambazo tunakabiliana nazo. Bwana wasamehe kwani hawajui wanachosema wala kufanya.

Seneta huyo wa zamani wa Nairobi alisema alikuwa ameshuhudia miujiza mingi maishani mwake na kwa hivyo, hatakata tamaa juu ya sala bila kujali watu walisema nini kumhusu.

Mwanasiasa huyo mwenye umri wa miaka 46 alimsihi Mungu awabariki maadui zake hata ikiwa walimtakia mambo mabaya maishani.

Habari Nyingine: Huyu Ndiye Mume wa Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, Hafidh Ameir

"Bwana mipango yoyote unayo kwa ajili yetu leo, tafadhali tubariki sisi sote pamoja na maadui zetu na wenye nia mbaya, tusaidie sisi wote kukuamini na kukutii kwa jina la Yesu."

Mike Sonko mnamo Disemba 3, 2020, alibanduliwa afisini na wawakilishi 88 wa wadi ya Nairobi kufuatia tuhuma za ukiukaji Katiba, matumizi mabaya ya ofisi na utovu wa nidhamu.

MCA wa Embakasi Michael Ogada ambaye pia ni kiongozi wa wachache katika bunge la Nairobi aliwasilisha hoja ambayo alielezea malalamishi dhidi ya Sonko.

Mjumbe wa Bunge la Kaunti (MCA) alimshtumu mkuu wa kaunti wakati huo kwa kuzamisha jimbo la Nairobi katika deni kubwa.

Habari Nyingine: Rais Samia Suluhu kulihotubia Bunge Wakati wa Ziara yake Nchini Kenya

Mnamo Disemba 17, 2020, Seneti iliunga mkono uamuzi wa bunge la kaunti kumfukuza mwanasiasa huyo kazini.

Baada ya kufutwa kazi, Sonko alisema alikuwa na furaha ya kurudia maisha yake ya zamani kabla ya kujiingiza katika siasa.

"Kama nilivyosema hapo awali, maisha lazima yataendelea hata baada ya siasa, na ninafurahi kurudia maisha yangu na kuwa na watu wa kawaida ambao wamekuwa wakiniunga mkono maisha yangu yote ya kisiasa," alisema.

Licha ya kukana madai kwamba alikuwa amegeuzwa kuwa bloga, mbunge huyo wa zamani wa Makadara mnamo Januari alisema anajiandaa kusomea uandishi wa habari baada ya kuwachana na siasa.

Read ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia news@tuko.co.ke au WhatsaApp: 0732482690.

Subscribe to watch new videos

Chanzo: TUKO.co.ke

ncG1vNJzZmijmajEorTIpaBnrKWgvG%2BvzmeinmdkZn15gJFmrpqrkaKyqbGMpqynn6ViwLC6yqhkmq%2BRpLqjscBmrpqjlaPGonnWmqWap52gsquxy6JksJmbnsCmucBmmKadm6rEonnBpaagmV6dwa64

 Share!