Magazeti ya Jumanne, Mei 12: Dhambi zilizomchochea Kipchumba Murkomen kupoteza wadhifa wake

Baada ya Rais Uhuru Kenyatta kumtupa nje Seneta wa Elgeyo Marakwet, Kipchumba Murkomen na mwenzake wa Nakuru, Susan Kihika kutoka kwa nyadhifa za Kiongozi wa Wengi Seneti na Kiranja wa Wengi, magazeti ya Jumanne, Mei 12 yanaripoti kuwa mabadiliko makubwa katika Bunge la Taifa na Baraza la Mawaziri huenda yakafuata.

Baada ya Rais Uhuru Kenyatta kumtupa nje Seneta wa Elgeyo Marakwet, Kipchumba Murkomen na mwenzake wa Nakuru, Susan Kihika kutoka kwa nyadhifa za Kiongozi wa Wengi Seneti na Kiranja wa Wengi, magazeti ya Jumanne, Mei 12 yanaripoti kuwa mabadiliko makubwa katika Bunge la Taifa na Baraza la Mawaziri huenda yakafuata.

Magazeti haya pia yanaongoza na habari kuhusu hatua ambazo taifa linapiga katika vita dhidi ya janga la COVID-19 huku idadi jumla ikifikia 700 siku ya Jumatatu, Mei 11.

Habari Nyingine: Padri taabani baada ya mpenziwe ambaye ni mke wa mtu kuaga dunia chumbani mwake

Habari Nyingine: Seneta Murkomen apokonywa gari saa chache baada ya kutemwa

1. People Daily

Licha ya Katibu Mkuu wa Chama cha Jubilee, Raphael Tuju kuonekana awali kama msaliti wa chama cha ODM, sasa ameibuka kuwa kipenzi cha chama hicho kinachoongozwa naRaila Odinga.

People Daily inaripoti kuwa Tuju amehusika pakubwa katika kubadilisha hatma ya kinara wa upinzani na huenda akaribishwe katika kambi ya Raila na shada la maua.

Mabadiliko ambayo Tuju ameshinikiza katika chama tawala yamewaacha wandani wa Naibu Rais William Ruto na funda chungu la mate.

Kwa upande mwingine, mabadiliko hayo yamekumbatiwa na ODM na hivyo kuwafanya wandani wa Ruto kumtaja Tuju kama kibaraka wa Raila katika Chama cha Jubilee.

2. Taifa Leo

Gazeti hili linaripoti kuwa maseneta Kipchumba Murkomen na Susan Kihika wameapa kuendelea kutekeleza wajibu wao kama Kiongozi wa Wengi Seneti na Kiranja wa Wengi mtawalia.

Wawili hao wamesema hawatambui mabadiliko ambapo nyadhifa zao zilitwaliwa na Seneta wa Pokot Magharibi, Samuel Poghisio na Seneta wa Murang'a, Irungu Kang'ata.

Kulingana na Murkomen na Kihika, mabadiliko hayo hayawezi kutekelezwa kwani hayakufuata katiba ya Chama Cha Jubilee.

3. The Star

Seneta wa Elgeyo Marakwet, Kipchumba Murkomen alinyanganywa gari la serikali katika Barabara ya Mombasa saa chache baada ya kupuuza mabadiliko ambayo ilimshuhudia akitemwa kutoka kwa wadhifa wake wa Kiongozi wa Wengi Seneti.

The Star inaripoti kuwa hatua hiyo pia inamsubiri Seneta wa Nakuru, Susan Kihika ambaye alibanduliwa kwenye wadhifa wake wa Kiranja wa Wengi Seneti.

Spika wa Seneti, Kenneth Lusaka anatazamiwa hii leo kuthibitisha ama kukataa mabadiliko hayo mapya ambayo yalitekelezwa katika Ikulu Jumatatu.

Kulingana na chapisho hili, Rais Uhuru Kenyatta amekuwa na mipango kwa muda ya kufanya mabadiliko na alianza kwa kubadilisha Kamati ya Kitaifa ya Uongozi wa Jubilee (NMC) na wanachama wake waaminifu.

4. The Standard

The Standard inajaribu kuelezea makosa ambayo Seneta Kipchumba Murkomen alifanya na kumpekelea kupoteza wadhifa wake wa Kiongozi wa Wengi Seneti.

Kulingana na gazeti hili, Murkomen alianza kupoteza kibali kwa uongozi wa Jubilee baada ya maafikiano ya mnamo Machi 2018 kati ya Rais Uhuru na kiongozi wa upinzani Raila Odinga.

Mbunge huyo amekuwa akitumia mamlaka yake katika Seneti kumshambulia Rais kutokana na uhusiano wake na Raila akidai kuwa ndio hisia ya watu wote wa Bonde la Ufa.

Murkomen pia alikuwa anamulikwa kwa kupinga ripoti ya Jopo Kazi la Maridhiano (BBI) na kukosa mkutano wa kwanza wa majadiliano Kisii.

Hata hivyo, baadaye alibadilisha msimamo na kusema anaunga mkono wito wa kura ya maamuzi wakati alihudhuria kampeni ya BBI iliyoandaliwa Mombasa.

5. Daily Nation

Wizara ya Afya imesema kuwa ili kuwalinda maafisa wa afya dhidi ya virusi vya corona, kila mmoja anayekwenda kutafuta matibabu hospitalini ni lazima apimwe virusi hivyo kabla ya kulazwa.

Haya yaliibuka mnamo Jumatatu, Mei 11, wakati visa vya COVID-19 nchini vilifika 700.

Maafisa wa afya walisema wanawafuatilia sana madereva wa lori ambao wanarekodi visa vingi.

Pia walitambua kuwa mipaka kwa mfano ya Namanga, Malaba, Mandera na Wajir imetambuliwa kuwa maeneo hatari.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia news@tuko.co.ke au WhatsaApp: 0732482690.

Subscribe to watch new videos

Chanzo: TUKO.co.ke

ncG1vNJzZmijmajEorTIpaBnrKWgvG%2BvzmeinmdjaoN1hJBmpJqfka%2BytbWMsphmoqWirq%2B6xGaknqFdZn9usMeapJuhXa%2B2rbXZqKScoJ%2BYtaatjKSgqZuYqrqjrYymrKujn6Kyr3nKrqeorJWvrm7DwJ2fop6RYsSit8Rnn62lnA%3D%3D

 Share!