Rais Uhuru amekubali naibu wake kushambuliwa, Ngunjiri asema

- Ngunjiri alisema Rais huwa anzama kwenye kicheko wakati DP analimwa kisiasa na viongozi waliosimama mbele yake - Alimtaka kumuonea DP huruma na ajiweke katika viatu vyake kwani yeye pia ni binadamu - Alisema kimya cha Rais ndicho kimetia mafuta kwenye moto unaoendelea kuchoma Jubilee

- Ngunjiri alisema Rais huwa anzama kwenye kicheko wakati DP analimwa kisiasa na viongozi waliosimama mbele yake

- Alimtaka kumuonea DP huruma na ajiweke katika viatu vyake kwani yeye pia ni binadamu

- Alisema kimya cha Rais ndicho kimetia mafuta kwenye moto unaoendelea kuchoma Jubilee

Mbunge wa Bahati Kimani Ngunjiri amemtaka Rais Uhuru Kenyatta kuwakataza wandani wake kumshambulia naibu wake William Ruto.

Akiongea va wanahabari Jumapili, Mei 2 akiwa nyumbani kwake Nakuru, Ngunjiri alisema Rais ndiye amewaruhusu marafiki wake kumpiga kisiasa Ruto bila yeye kusema lolote.

Habari Nyingine: Jumapili, Mei 3: Kenya yarekodi visa vingi zaidi vya coronavirus, wawili wafariki

"Nauliza Uhuru Muigai Kenyatta, Atwoli anasimama mbele yako na kuongea kumshambulia Ruto na kupigia kampeni BBI, na wewe ni kucheka tu. Ukisimama huwezi sema lolote," Ngunjiri alisema.

Mbunge huyo alihoji ni kwa nini Uhuru yuko kimya wakati ambapo wandani wake wanamshambulia DP na pia kuhusu mzozo wa chama cha Jubilee.

"Kwa nini usisimame na kusema hutaki hii mambo? Wewe ni kucheka tu, DP wako akipigwa," aliongeza.

Habari Nyingine: Mbuzi na papai walipatikana kuwa na coronavirus, Magufuli asema

Alimtaka Rais kufikiria iwapo anayoyapitia Ruto, huku rais akiwa kimya, yangemkumba yeye angejihisi vipi.

"Kama ni wewe ungekuwa naibu rais, na Ruto awe rais alafu ufanyiwe yale mnafanyia Ruto. Kuweka watu wa kushambulia yeye kutoka afisi yako, ungehisi vipi?

"Ruto ni mtu, yuko na familia ...yuko na mama ....ako na jamii yake na mama yake ni kama mama yako. Unafikiria anahisi vipi akiona vile mnafanyia yeye? aliongeza Ngunjiri.

Habari Nyingine: Mwathethe azungumza baada ya Rais Uhuru kutangaza mabadiliko kwenye uongozi wa jeshi

Wandani wa Rais kama vile David Murathe wamekuwa wakimshambulia DP wakiahidi kuhakikisha hajafaulu kisiasa.

Urafiki wa DP na Rais umeonekana kufifia huku uongozi wa chama chao nao ukiyumba pakubwa kutokana na mabadiliko yaliyofanywa bila kuhusisha pande zote.

Katibu Raphael Tuju alifanya mabadiliko ambayo yalipingwa na DP Rutona kundi lake la wabunge.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia news@tuko.co.ke au WhatsaApp: 0732482690.

Subscribe to watch new videos

Chanzo: TUKO.co.ke

ncG1vNJzZmijmajEorTIpaBnrKWgvG%2BvzmeinmdjaoF6gpJmqZqho2LCqcHRrmSapZWgwqOty6Jkp5mZl8Juw8CknGajpai1ornBrqOir5Fiu6jBzaOgq6FdlsCmucBnn62lnA%3D%3D

 Share!