Meru: Wazee wa Njuri Ncheke kusawazisha mahari kwa wasichana wote

Wazee wa Njuri Ncheke wameapa kuunda sheria ambayo itasawazisha mahari inayolipwa na wakazi wa Meru na Tharaka Nithi. Wazee hao walikubaliana haya wakati wa mkutano na Gavana wa Meru Kiraitu Murungi Jumatano, 2 Octoba.

Wazee wa Njuri Ncheke wameapa kuunda sheria ambayo itasawazisha mahari inayolipwa na wakazi wa Meru na Tharaka Nithi.

Wazee hao walikubaliana haya wakati wa mkutano na Gavana wa Meru Kiraitu Murungi Jumatano, 2 Octoba.

Habari Nyingine: Vyakula na vinywaji kutoka nje vyapigwa marufuku SGR

Wazee hao wamesema kuwa wananume wamekuwa wakikabiliwa na wakati mgumu kuwaoa wasichana kutokana na mahari ghali ambazo wazazi wamekuwa wakiitisha kwa mujibu wa Nairobi news.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya mkutano huo, Katibu wa Njuri Ncheke Josphat Marangiri alisikitika jinsi wazazi wa kisasa wameweka tamaa mbele na kufanya mahari kama biashara.

Marangiri alisema enzi zile, wazazi wa mume walikuwa wanalipa mbuzi mmoja wa kike, kifurushi cha miraa, asali, ndama, ng'ombe dume, kondoo, blanketi kama zawadi kwa mamake msichana na koti la babake.

Habari Nyingine: Ujumbe wa Rayvanny kwa bosi wake Diamond Platnumz akitumu miaka 30

Hata hivyo, Njuri Ncheke walisema mume aliruhusiwa kumuoa msichana baada ya kukamilisha malipo ya mbuzi ama miraa huku mengine akitakiwa kulipa polepole.

"Mume alitakiwa kumzawadi mamake binti blanketi na koti kwa baba. Siku hizi watu wanaitisha suti, viatu na bidhaa nyingine ghali mno ambazo haziambatani na desturi zetu," Murangiri alisema.

Aliongeza kuwa, bidhaa hizo zenye bei ghali zinawaingiza uoga wanaume ambao wanashindwa kuoa kwa njia inayostahili.

Habari Nyingine: Mwanga wa Kiswahili: Ukuzaji lugha kupitia maonesho ya vitabu na tuzo za waandishi

Wazee hao walikubaliana kupendekeza kiasi fulani cha hela ambacho kila mume atakuwa akilipa kama mahari, pasi na wazazi kuongeza wala kupunguza.

Gavana Murungi alikubaliana na wazee hao na kuwataka kuunda sheria ambazo kila familia itastahili kufuata akisema kuwa bei ya mahari imepanda na kuwazuia vijana kutoka Meru kuoa.

Gavana alisema baadhi ya wazazi wamepandisha bei ya mahari na kudokeza kuwa hatua ya kusawazisha kiasi cha mahari inayostahili kulipwa itawarahisishia mzigo vijana hususan wale ambao hawajiwezi kifedha.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia news@tuko.co.ke au WhatsApp: 0732482690.

Subscribe to watch new videos

Chanzo: TUKO.co.ke

ncG1vNJzZmijmajEorTIpaBnrKWgvG%2BvzmeinmdjZoR0f5RmpJ6qpWLEosbEnmSwmV2jt7a%2ByGalnKCVoLJut9SsmLCZqp7Aqa2MppihmaKeeqzDwGaumquZmLWiusBmrqislWO1tbnL

 Share!